Psalms 32:1-6

Furaha Ya Msamaha

(Utenzi: Zaburi Ya Daudi. Funzo)


1 aHeri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake,
ambaye dhambi zake zimefunikwa.

2 bHeri mtu yule ambaye Bwana
hamhesabii dhambi,
na ambaye rohoni mwake
hamna udanganyifu.


3 cNiliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa
kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.

4 dUsiku na mchana
mkono wako ulinilemea,
nguvu zangu zilinyonywa
kama vile katika joto la kiangazi.

5 eKisha nilikujulisha dhambi yangu
wala sikuficha uovu wangu.
Nilisema, “Nitaungama
makosa yangu kwa Bwana.”
Ndipo uliponisamehe
hatia ya dhambi yangu.


6 fKwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe
wakati unapopatikana,
hakika maji makuu yatakapofurika
hayatamfikia yeye.
Copyright information for SwhKC