Psalms 32:1-6
Furaha Ya Msamaha
(Utenzi: Zaburi Ya Daudi. Funzo)
1 aHeri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake,
ambaye dhambi zake zimefunikwa.
2 bHeri mtu yule ambaye Bwana
hamhesabii dhambi,
na ambaye rohoni mwake
hamna udanganyifu.
3 cNiliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa
kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.
4 dUsiku na mchana
mkono wako ulinilemea,
nguvu zangu zilinyonywa
kama vile katika joto la kiangazi.
5 eKisha nilikujulisha dhambi yangu
wala sikuficha uovu wangu.
Nilisema, “Nitaungama
makosa yangu kwa Bwana.”
Ndipo uliponisamehe
hatia ya dhambi yangu.
6 fKwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe
wakati unapopatikana,
hakika maji makuu yatakapofurika
hayatamfikia yeye.
Copyright information for
SwhKC